TUNAKUTUKUZA

TUNAKUTUKUZA ndio Toleo la hivi karibuni la maombi, nyimbo na ibadakutoka kwa Dkt. Noel Woodroffe na Kiwanda cha Muziki cha Congress.

Dhihirisho hili kuu la kuabudu linatiririka kutoka kwa moyo wenye shukrani wa watu duniani kote wanaosherehekea ukuu, utawala na utukufu wa Mungu na kudhihirisha maadili, tabia na asili yake hapa duniani.

Albamu hii inawakilisha hatua muhimu katika safari yetu ya pamoja. Toleo la lugha ya Kiingereza lilifanywa katika kikao spesheli cha kurekodi katika Elijah Centre, Kiini Bunifu cha Congress. Kikao hiki kiliongozwa na Dkt. Woodroffe na mke wake Dada June na kilijumuisha watakatifu kutoka Elijah Centre pamoja na waakilishi teule kutoka kwa Mtandao wa Jamii {KCN}walio Trinidad na Tobago.

Waimbaji na wanamuziki kutoka ulimwengu wetu baadaye walijiunga pamoja ili kutengeneza raslimali hii katika takriban lugha kumi na nne. Sasa, sauti za watakatifu kutoka duniani kote zinaweza sikika zikiinua sauti nzuri ya sifa na ya kuabudu kwa Bwana wetu Yesu Kristo.